Tuesday, July 15, 2014

MBRAZIL MWINGINE ATUA YANGA

Timu ya soka ya dar-es-salaam young africans imemsajili mshambuliaji Geilson Santos Santana "jaja" kutoka Brazil,jaja mwenye miaka 28 aliyekua akiichezea klabu ya itabaina FC ya brazil anakua mchezaji wa pili kutoka nchini brazil kusajiliwa na yanga mchezaji huyo amewasili leo mchana akitokea sao paulo nchini brazil hivyo ataungana na  wabrazil wenzie makocha Marcio maximo na  Leonardo neiva pamoja na mchezaji Andrey coutinho,yanga wamefanya usajili huo ili kuimarisha kikosi chao kwa ajili ya michuano ya kombe la kagame itakayofanyika Kigali nchini Rwanda,ligi kuu ya vodacom Tanzania bara pamoja na michuano ya kombe la shirikisho barani africa.

No comments:

Post a Comment