Klabu ya arsenal imefanikiwa kunasa saini ya beki wa kulia wa Newcastle united Mathieu debuchy raia wa ufaransa kwa kitita cha paundi milioni 12 debuchy amesajiliwa na arsenal ili kuziba pengo la beki wa kulia lililoachwa na mfaransa mwenzie bacary sagna aliyetimkia manchester city debuchy amesema "nimefurahi kujiunga na arsenal sababu ni moja kati ya timu kubwa duniani na ninaahidi kuisaida kunyakua mataji mbalimbali" naye kocha wa arsenal arsene wenger amesema ana imani uzoefu wa debuchy utaisaidia arsenal kufanya vizuri msimu ujao.
No comments:
Post a Comment